BREAKINGNEWS:Mwanajeshi apigwa risasi mkoani Njombe. - HD NEWS

Breaking

Habari za Uhakika

Socialize

Thursday

BREAKINGNEWS:Mwanajeshi apigwa risasi mkoani Njombe.



Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika kikosi cha Makambako (KJ 514) ambaye amefahamika kwa jina la Neema Masanja amefariki dunia baada ya kupigwa risasi na mchumba wake ambaye ni askari wa Jeshi la Polisi Makambako mkoani Njombe.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Prudensiana Protas amethibitisha kutokea kwa tukio hilo mapema jana na kusema kuwa Askari wa jeshi la polisi Makambako mkoani Njombe ambaye anafahamika kwa jina la Zakayo Dotto alifanya tukio hilo la mauaji kwa kile kinachodaiwa kuwa ni wivu wa mapenzi.

Jeshi la Polisi linaendelea na msako wa kumtafuta mtuhumiwa Zakayo  Dotto ambaye baada ya kufanya tukio hilo la mauaji alikimbia kusikojulikana.

No comments:

Post a Comment